6. Wakristo, iwekeni

1 Wakristo, iwekeni
mioyo tayari.
Yesu awaingie,
ni Mwokozi wenu.
Mungu amemtuma
kwa neema na rehema
atuletee sisi
uzima na nuru.

2 Mwokozi anakuja,
mlimieni njia!
Mioyo iwe safi
acheni matendo
yanayomchukiza.
Lijazwe kila bonde,
milima ipunguzwe
mioyoni mwenu.

3 Ukiwa mnyenyekevu,
Wapendwa na Mungu.
Ukiwa na kiburi,
utaangamizwa.
Ukimtumikia
Mungu kwa Mwendo mwema
umpendezao yeye,
Yesu akupenda.

4 Uniwke tayari,
niliye maskini,
Ee Yesu, siku hizi
kwa rehema yako,
Ingia moyoni,
ukinijia sasa.
Nami nitakusifu
kwa kinywa na moyo.

Text Information
First Line: Wakristo, iwekeni
Title: Wakristo, iwekeni
German Title: Mit Ernst, o Menschenkinder
Author: V. Thilo, 1607-1662
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Notes: Sauti yake: Namba 206; Posaunen Buch, Erster Band #5 and #94
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us