Text: | Mwenzetu, kazi yako |
Author: | Hajulikani |
1 Mwenzetu, kazi yako
imekwisha duniani.
Umekwisha kutua
mzigo wa shida na taabu.
Yesu tupe kufika
walipo washindaji.
2 Yesu ni kiongozi
katika bonde la kufa.
Amekutangulia
kaburini na peponi.
Yesu tupe kufika
walipo washindaji.
3 Wewe wachukuliwa
na malaika kwa Mwokozi.
Utapokewa sasa
na wateule wa Mungu.
Yesu tupe kufika
walipo washindaji.
4 Mwili wako wazikwa,
ugeuke kuwa vumbi.
Twatumaini kwamba
ufufuko utakuwa.
Yesu tupe kufika
walipo washindaji.
5 Sasa unapandwa tu
kama mbegu ya shambani.
Mpaka yaje mavuno
siku ya kufufuliwa.
Yesu tupe kufika
walipo washindaji.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Mwenzetu, kazi yako |
Title: | Mwenzetu, kazi yako |
Author: | Hajulikani |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kufa na kuzikwa |
Notes: | Sauti: Posaunen Buch #29, Nyimbo za Kikristo #153 |