199. Sijui saa ya kufa kwangu

1 Sijui saa ya kufa kwangu,
maisha yangu yapita.
Naomba: Mungu,
Bwana wangu
kwa ajili ya Mwanao.
Shika roho yangu,
kwa furaha,
niache ulimwengu huu.

2 Tukiwa hapa duniani
kufa kunatuvizia,
hakutuwekei kiaga,
hunakuja kwa haraka.
Shika roho yangu,
kwa furaha,
niache ulimwengu huu.

3 Unifundishe nifikiri
vizuri mambo ya kufa,
nijutie makosa yangu,
yaondolewe na Yesu.
Shika roho yangu,
kwa furaha,
niache ulimwengu huu.

4 Unipe nguvu, nijiweke
tayari kwa mambo yote,
niweze kuitikia vema,
ukiniita kwa kufa.
Shika roho yangu,
kwa furaha,
niache ulimwengu huu.

5 Baba, ondoa dhambi zangu
kwa damu ya Bwana Yesu,
najificha katika huyu,
kwani amenikomboa.
Shika roho yangu,
kwa furaha,
niache ulimwengu huu.

6 Nikiwa naye Bwana Yesu,
sioni hofu kwa kufa.
Na saa ya kufa ikifika,
namtumaini Yesu tu,
Ninajua: Kwa damu ya Yesu
napata kufa kuzuri.

Text Information
First Line: Sijui saa ya kufa kwangu
Title: Sijui saa ya kufa kwangu
German Title: Wer Weiss wie nahe mir mein Ende
Author: A. J. v. Schwarzburg-Rudolstadt, 1637-1706
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kufa na kuzikwa
Notes: Sauti: Wer weiss wie nahe mir mein Ended, Asili: F. V. Buttstedt 1744, Posaunen Buch #68
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us