126. Karibu kwangu Roho

1 Karibu kwangu Roho
ingia moyoni,
uliyeniletea uzima na raha.
Roho Mtakatifu
wa Baba na wa Mwana
ufananaye nao
ukaaye nao.

2 Unafundish watu
kuomba vizuri,
wapate kusikiwa
na Mungu mbinguni.
Unatuombea,
hukomi, mpaka Mungu
atende mambo yale
uliyoyaomba.

3 Wafurahisha moyo,
hupendi huzuni;
tukiwa matesoni,
unatutuliza.
Wazungumza nasi
Kwa neno lko tamu,
unatia mioyo
furaha ya kweli.

4 Unatufanya sisi
kuwa usharika;
hutaki tugombane
na kuchukiana.
Wanaopigana
unawapatanisha;
wataka wapendane
Wakristo wowote.

5 Umlinde Rais wetu,
serikali yetu,
tukae na amani
duniani humu.
Uwape wakubwa,
pamoja na wadogo
uchaji na akili,
wampendeze Mungu.

6 Katika mwendo wetu
utupe na sisi
nguvu, tumshinde mwovu
akitujaribu.
Utusaidie,
tushike njia yako
na mwisho tufe vema
tufike kwa Mungu.

Text Information
First Line: Karibu kwangu Roho
Title: Karibu kwangu Roho
German Title: Höchster Tróster komm hernieder
Author: D. Bruhn (1782)
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Yesu anawapa wanfunzi wake Roho Mtakatifu
Notes: Sauti: Höchster Trúoster komm hernieder, Posaunen Buch, Erster Band #5
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us