Hymnal: NzIY2003 #2 (2003) Person Name: John B. Dykes 1823-1876 First Line: Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi Lyrics: 1 Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,
Kila tukiamka tunakuabudu.
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi,
Ewe Utatu, tunakusifu.
2 Baba, Mwana, Roho, wakuaminio,
Wanakutolea shukurani zao.
Wakusujudia malaika nao:
Wewe U mwanzo, nawe U mwisho.
3 Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani,
Utukufu wako makosa hauna,
U Mtakatifu, nawe U mapenzi,
U peke yako, mwenzio huna.
4 Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,
Ulivyoviumba vyote vyakusifu:
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi,
Ewe Utatu, tunakusifu.
Languages: Swahili Tune Title: NICAEA
Baba, Mwana, Roho