161. Bwana twakuletea

1 Bwana, twakuletea
mtoto huyu, tukijua
(watu hawa, tukijua)
amri yako ya mwisho
uliyowapa mitume:
Watu wote wabatizwe,
watakaokuwa wako.

2 Neno hili ni kubwa
tulilopewa na Yesu:
Atakaye kufika
katika ufalme wako,
hana budi kuzaliwa
tena kwa maji na Roho.

3 Pokea kondoo wako
mchunga mwema Bwana Yesu.
Umwongoze mbinguni.
(Waongoze mbinguni,)
ndiwe njia na uzima.
Umpe kukutegema.
(wape kukutegemea,)
apate kutengemana.
(wapate kutengemana.)

4 Baba, tunakushi
ukubali wimbo wetu,
usikie maombi
tunayokuyomba sasa.
Andika jina la mtoto,
(Andika majina yao)
katika kitabu chako!

Text Information
First Line: Bwana, twakuletea
Title: Bwana twakuletea
German Title: Liebster Jesu, wir sind hier
Author: B. Schmolk, 1672-1737
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Ubatizo
Notes: Sauti asili: Ja er ist's das Heil der Welt by J. R. Ahle, 1664, Posaunen Buch #32
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us